LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

 

 

 

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie

Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie

Kristo utusikie Kristo utusikilize

Baba wa mbinguni Mungu Utuhurumie

Mwana, Mkombozi wa dunia Mungu Utuhurumie

Roho Mtakatifu Mungu Utuhurumie

Utatu Mtakatifu Mungu mmoja Utuhurumie

Moyo wa Yesu Mwana wa Baba wa Milele Utuhurumie

Moyo wa Yesu uliotungwa na Roho Mtakatifu mwilini mwa Mama Bikira Maria Utuhurumie

Moyo wa Yesu ulioungana na Neno wa Mungu Utuhurumie

Moyo wa Yesu ulio na utukufu pasipo mfano Utuhurumie

Moyo wa Yesu, hekalu takatifu la Mungu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, hema la Yule aliye juu Utuhurumie

Moyo wa Yesu tanuru lenye kuwaka mapendo Utuhurumie

Moyo wa Yesu, nyumba ya Mungu na mlango wa Mbingu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, tanuru yenye kuwaka mapendo Utuhurumie

Moyo wa Yesu, chombo cha haki na upendo Utuhurumie

Moyo wa Yesu, unaojaa upendo na wema Utuhurumie

Moyo wa Yesu, kilindi cha fadhila zote Utuhurumie

Moyo wa Yesu, unaostahili sifa zote Utuhurumie

Moyo wa Yesu, unaotawala mioyo yote Utuhurumie

Moyo wa Yesu, zinamokaa hazina za hekima na elimu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, uliopendelewa na Mungu Baba Utuhurumie

Moyo wa Yesu, uliotuenezea maziada yake Utuhurumie

Moyo wa Yesu, mtamaniwa wa vilima vya milele Utuhurumie

Moyo wa Yesu, wenye uvumilivu na huruma nyingi Utuhurumie

Moyo wa Yesu, tajiri kwa wote wenye kukuomba Utuhurumie

Moyo wa Yesu, chemchemi ya uzima na utakatifu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, malipo kwa dhambi zetu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, ulioshibishwa matusi Utuhurumie

Moyo wa Yesu, uliovunjika kwa sababu ya ubaya wetu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, uliotii mpaka kufa Utuhurumie

Moyo wa Yesu, uliochomwa kwa mkuki Utuhurumie

Moyo wa Yesu, chemchemi ya faraja zote Utuhurumie

Moyo wa Yesu, uzima na ufufuo wetu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, amani na upatanisho wetu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, sadaka ya wakosefu Utuhurumie

Moyo wa Yesu, unamokaa wokovu wao wenye kukutumaini Utuhurumie

Moyo wa Yesu, matumaini yao wenye kuzimia kwako Utuhurumie

Moyo wa Yesu, sababu ya furaha ya watakatifu wote Utuhurumie

Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusamehe Bwana

Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusikilize Bwana

Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utuhurumie

Kiongozi: Yesu mwenye Moyo mpole na mnyenyekevu,

Wote: Ufanye mioyo yetu ifanane na Moyo wako

TUOMBE: (W) Ee Mungu Mwenyezi milele, uuangalie Moyo wa mwanao mpendelevu, pia na heshima na malipo aliyokutolea kwa ajili ya wenye dhambi, uridhike, uwaondolee wenye kuomba toba kwako kwa njia ya huyo Mwanao Yesu Kristo anayeishi na kutawala nawe pamoja na Roho Mtakatifu, Mungu milele. Amina.

Comments

Popular posts from this blog

Litania Ya Huruma ya Mungu

LITANIA KWA MT RITA WA KASHIA

Kusali Rozari Nzima: Maana, Faida, na Jinsi ya Kusali