Sala ya Usiku


Sasa siku imekwisha,

Kwako Mungu napandisha,

moyo wangu kwa shukrani,

nipumzike kwa amani,


Mema mengi umenipa,

ninashindwa kukulipa,

Baba mwema ondolea,

yote niliyokosea.


Yesu mpenzi unijie,

ombi langu usikie,

unifiche mtoto wako,

ndani ya jeraha zako,


Ewe Mama unipe neema,

raha na usiku mwema,

Roho mlizi ukakeshe,

pepo wasinikoseshe


Naiweka roho yangu,

mikononi mwa Baba yangu,

bila hofu napumzika,

mwisho kwake nitafika.


Amina


Comments

Popular posts from this blog

Litania Ya Huruma ya Mungu

LITANIA KWA MT RITA WA KASHIA

Kusali Rozari Nzima: Maana, Faida, na Jinsi ya Kusali