Sala ya Asubuhi


Ee Baba yetu Mungu Mkuu,

Umenilinda usiku huu,

Ninakushukuru kwa moyo,

Ee Baba, Mwana na Roho,

Nilinde tena siku hii,

Niache dhambi nikutii,

Naomba sana Baba wee,

Baraka yako nipokee,

Bikira safi ee Maria,

Nisipotee unisimamie,

Mlinzi Mkuu Malaika wee,

Kwa Mungu wetu niombee,

Nitake nitende mema tu,

Na mwisho nije kwake juu.

Comments

Popular posts from this blog

Litania Ya Huruma ya Mungu

LITANIA KWA MT RITA WA KASHIA

Kusali Rozari Nzima: Maana, Faida, na Jinsi ya Kusali