Sala ya Asubuhi


Siku mpya inaanza ,

nimwabudu Mungu kwanza

Mungu wangu baba yangu,

upokee shukrani zangu

Wewe kwa usiku mzima,

ulikuwa kwangu daima

Kunilinda kwa amani,

na mitego ya shetani

Kwako baba wa milele,

ninaomba neema tele

Niepuke dhambi zote,

nikutumikie kote

Ubariki kazi yangu,

shida na furaha zangu

Mama safi eeh Maria,

nipe msaada wako pia

Malaika kiongozi,

nipeleke kwa mwokozi

Yesu nijalie neema

niwe daima mkristo mwema


Amina

Comments

Popular posts from this blog

Litania Ya Huruma ya Mungu

LITANIA KWA MT RITA WA KASHIA

Kusali Rozari Nzima: Maana, Faida, na Jinsi ya Kusali