Nia Njema


Kumheshimu Mungu wangu

Namtolea roho yangu,

Nifanye kazi nipumzike

Amri zake tu nishike

Wazo, neno, tendo lote

Namtolea Mungu pote

Roho, mwili chote changu,

Pendo na uzima wangu

Mungu wangu nitampenda,

Wala dhambi sitatenda.

Jina lako nasifia,

Utakalo hutimia.

Kwa utii navumilia

Teso na matata pia.

Nipe, Bwana, neema zako

Niongeze sifa yako.

Amina.

Comments

Popular posts from this blog

Litania Ya Huruma ya Mungu

LITANIA KWA MT RITA WA KASHIA

Kusali Rozari Nzima: Maana, Faida, na Jinsi ya Kusali