Kanuni ya Imani


Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, mwumba mbingu na dunia.

Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,

akazaliwa na Bikira Maria,

akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato,

akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu;

siku ya tatu akafufuka katika wafu;

akapaa mbinguni; amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi;

toka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu.

Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,

Kanisa takatifu katoliki,

ushirika wa Watakatifu,

maondoleo ya dhambi,

ufufuko wa miili, uzima wa milele.

Amina.


Comments

Popular posts from this blog

Litania Ya Huruma ya Mungu

LITANIA KWA MT RITA WA KASHIA

Kusali Rozari Nzima: Maana, Faida, na Jinsi ya Kusali